Tume ya Ushindani (FCC) yakutana na Uongozi wa Chama cha Mawakala wa Mizigo Tanzania (TAFFA) ili kujadili mambo mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa Sheria ya Alama za Bidhaa ikiwa ni pamoja na kuboresha na kutatua kero zinazoweza kujitokeza katika utekelezaji wa majukumu hayo.
Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw. William Erio amesema kuwa kwa mwaka huu Tume itajikita katika utoaji wa elimu kwa wadau wa biashara na waingizaji wa bidhaa ili kupunguza changamoto zinazohusiana na masuala ya alama za bidhaa.

Kikao hiki ni muendelezo wa FCC kukutana na wadau wake na kujadili namna bora ya matumizi ya alama za bidhaa, kuweka mazingira wezeshi ya kibiashara na kushajiisha ushindani katika soko.
Kwa upande wake akizungumza kwa niaba ya TAFFA Bw. Waheed Saudin, Makam wa Rais wa TAFFA ameishukuru FCC kwa kuwa na desturi ya kuwaita wadau wake, kukaa pamoja na kujadili namna mbalimbali za kuweka mazingira wezeshi ya kibiashara ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika mazingira ya kibiashara.

Kikao hiki kimefanyika tarehe 17 Januari, 2025 katika ofisi ya FCC Dar es Salaam.












 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...