Na Mwandishi Wetu

OFISI ya Diwani Kata ya Kivukoni jijini Dar es Salaam imetoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani sambamba na kukata keki kwa ajili ya kusherehekea Happy Birthday ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.

Usomwaji wa taarifa hiyo ya utekelezaji wa Ilani pamoja na kukata keki ya Rais umefanyika leo Januari 26,2025 jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo akiwemo Mwenyekiti wa CCM Mkoa Abbas Mtemvu.

Wengine waliohudhuria ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Alhaji Said Sidde pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa na Naibu Spika Wa Bunge Mhe Mussa Azzan Zungu pamoja na Wajumbe wa NEC Mkoa akiwemo Juma
Gafafi.
 

Katika usomaji wa utekelezaji wa Ilani ofisi ya Diwani Kata ya Kivukoni ambayo Diwani wake ni Sharik Choughule imejivunia utekelezaji wa Ilani kwani kuna miradi mingi ya maendeleo imefanya na kutumia nafasi hiyo kumpongeza Rais Dk.Samia kwa kuhakikisha anasimama imara oufanikisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2020-2025.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...