RAIS Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Chakula Afrika (Africa Food Prize Committee) na Mjumbe wa Bodi ya AGRA, anashiriki Mikutano mbalimbali kuhusu uboreshaji wa kilimo barani Afrika, kuelekea kupitishwa kwa Programu ya Kuendeleza Kilimo Barani Afrika (CAADP 2026 - 2035), Kampala, nchini Uganda.
Mikutano hii itafikia kilele kwa kupitishwa kwa Azimio la Kampala, na mkakati wa kihistoria wa miaka kumi na mpango kazi, ili kuimarisha utekelezaji wa Azimio la Malabo kuhusu Ukuaji wa Kasi wa Kilimo na Mabadiliko kwa Ustawi wa Pamoja na Maisha Bora, lililopitishwa mwaka 2014.
.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...