
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi hiyo uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Januari, 2025.
Katika Mkutano huo, Mhe. Rais Dkt. Samia alishiriki pamoja na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema sambamba na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera. Aidha, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi walishiriki kwa njia ya mtandao.



Katika Mkutano huo, Mhe. Rais Dkt. Samia alishiriki pamoja na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema sambamba na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera. Aidha, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi walishiriki kwa njia ya mtandao.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...