-Mosi Aagiza Eneo la Feri kuwa Safi


-Pili Mchakato wa kumpata Mwekezaji Mkubwa wa dampo uharakishwe


-Tatu Barabara ya Feri kwenda Hyatt, Johari Rotana mpaka stesheni itafungwa kwa baadhi ya vyombo vya usafiri 


-Nne Katibu Tawala wa Mkoa kusimamia watendaji wote kuanzia TPA, Temesa kuja Jiji maeneo hayo yawe safi


-Tano Barabara zitakazotumiwa na Marais kwa ajili ya mazoezi ziwashwe taa


-Sita Kibaka yoyote atakayekamatwa apelekwe maabara


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila Leo tarehe 11 Januari 2025 ameshiriki katika zoezi Maalumu la usafi wa Mji pamoja na Vyombo vya Usalama, Viongozi wa Mkoa, Wilaya, Halmashauri na Taasisi za Umma lililofanyika katika Wilaya ya Ilala.


Akiwa katika zoezi Maalumu la Usafi RC Chalamila ametoa Maelekezo *Sita* ya kuzingatia kuelekea Maandalizi ya ujio wa Marais wa Afrika ikiwa ni pamoja na:-


Mosi, Eneo la feri linapaswa  kuwa safi ambapo Mhe. Chalamila amesema Soko Hilo kwa muda mrefu  limekuwa haliridhishi katika usafi hivyo kama atagundua bado hali ni mbaya tarehe 23- 25 atapafunga  na kuwaleta  Jeshi,  Polisi, Jkt, Zimamoto, Uhamiaji watafanya usafi mpaka pale watakapojifunza wafanyabiashara hao namna ya  kufanya biashara na kutunza mazingira


Hata hivyo Mkuu wa Mkoa ameagiza Mchakato wa kumpata Mwekezaji Mkubwa wa Dampo uharakishwe mara Moja ili dampo lipate mwekezaji Mkubwa anayejitambua anayeweza kuzalisha ajira, gesi, na mbolea


Vile vile RC Chalamila ameongeza kuwa Barabara ya feri kwenda hyati, Johari Rotana   mpaka stesheni  itafungwa *kwa baadhi ya vyombo vya usafiri* na kuelekezwa vipite wapi  ili wageni wetu watakapokuwa hapa kusiwe na foleni kubwa


Aidhaa, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemuagiza Katibu Tawala kuwasimamia  watendaji wote wa maeneo ya  kuanzia TPA kuja Temesa kuelekea Jiji kuwa yawe safi 


Wakati huo huo RC Chalamila amesisitiza kuwa Barabara zitakazotumiwa na Marais kwa ajili ya mazoezi  ziwashwe taa ili vibaba wadogo wadogo waweze kuwa na aibu kutokana na taa zinazowaka


Mwisho Mhe.Chalamila akasisitiza kuwa kibaka wote kuanzia Leo atakayekamatwa apelekwe maabara ili kiwe chombo Cha kufundishia kwa wanafunzi wanaotaka kuja kuwa wezi (watakaojifunza kuwa wizi haustahili katika Jiji la Dar es Salaam).













*#Dar es Salaam Safi inaanza na mimi#*

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...