Na. Mwandishi wetu - Saudi Arabia

Serikali imekemea watanzania wanao kwenda kufanya kazi nje ya nchi bila kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria kwa kuwa inasababisha kutojulikana walipo na shughuli wanazozifanya.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa utekelezaji wa makubaliano ya kuwezesha na kuratibu Ajira za Watanzania nchini Saudi Arabia leo Januari 27. 2024. 


Aidha, amesema uhusiano mazuri uliopo baina ya Tanzania na nchi ya Saudi Arabia hawataruhusu wafanyakazi kufanya kazi au kusafiri bila kufuata utaratibu, hivyo kila mtanzania anayehitaji kufanya kazi nje ya nchi apitie kwa mawakala wanatambulika baina ya nchi hizo mbili.

Mhe. Ridhiwani amesema miongoni mwa makubaliano yaliyofikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa watanzania kusafiri kwenda nchini Saudi Arabia, upimaji wa Afya zao, kupata kazi zenye staha na mshahara mzuri ambao utawasaidia kujikwamua kiuchumi.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...