Shirika la Umeme Tanzania, TANESCO, linashiriki katika Maonesho kando ya Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi wa Afrika (African Energy Summit) unaofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC).

Mkutano huo umeanza leo Januari 27, 2025 unawakutanisha Wakuu wa Nchi Barani Afrika kujadili mikakati ya upatikanaji wa nishati ambapo lengo kuu ni kuwafikishia nishati ya umeme Waafrika milioni 300 ifikapo mwaka 2030.

TANESCO kama mdau muhimu wa nishati ya umeme hapa nchini imeendelea kutumia maonesho hayo kutoa elimu kwa wadau juu ya matumizi ya nishati ya umeme ikiwa ni pamoja na maendeleo ya miradi ya umeme na matumizi ya nishati safi ya umeme kupikia.

Mkutano huo utamalizika kesho Januari 28, 2025 ambapo unatarajiwa kuonyesha mwelekeo wa mpya nishati katika bara la Afrika.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...