MWENYEKITI Mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni Mjumbe wa Kudumu wa Kamati Kuu ya Chama hicho, Freeman Mbowe anatoa maagizo kwa viongozi wapya wa chama hicho kuunda tume kwa ajili kuyaponya majeraha yaliyotokana na kampeni za uchaguzi uliomuondoa madarakani.

Mbowe ameyasema hayo leo tarehe 22 Januari 2025 alipokuwa akiwaaga wajumbe na wanachama wa chama hicho mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa Chama katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

"Kwa namna wagombea mbalimbali walifanya kampeni zao zimeacha majeraha mengi, tusipolitibu jambo hili litaharibu brand ya chama chetu".

"Mimi niliahahidi nikishinda nitaunda tume ya kuponya majeraha yaliyotokana na uchaguzi, nazungumza kama Baba wa Chama hiki, nawaagiza katibuni majeraha haya undeni tume haraka ya kuponya majeraha" Ameeleza Mbowe.

Aidha amewahasa viongozi hao kutokufanya jambo jambo kinyume cha Katiba ya chama hicho.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...