MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Chama Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wassira, ameiagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kuhakikisha ardhi ya vijiji iliyoporwa kinyume cha sheria, inarudishwa kwa wananchi.

Wasira alitoa maagizo hayo leo jijini Dodoma, wakati akizungumza na viongozi pamoja na wanaCCM waliojitokeza kumpokea katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM.

Alisema kuna watu wamejimilikisha ardhi kwa kutoa rushwa jambo ambalo CCM inaakataa kwa nguvu zake zote.

“Haki ya Watanzania kumiliki ardhi ni sera ya msingi kwa CCM. kuna watu wanajimilikisha maeneo makubwa na hawayaendelezi kwa kutoa rushwa. Tunaomba maeneo yote ambayo yanamilikiwa kinyume cha sheria yarudishwe kwa wananchi,” alisisitiza.

“Tunataka kuona watu wakipata matatizo sehemu yao sahihi ambayo wanaweza kupata ufumbuzi iwe CCM. Hivyo tunaendelea kuhamasisha kuwa kitu kimoja. Hii ni muhimu hasa kipindi hiki tunapoelekea katika uchaguzi mkuu, lazima tuungane ili tushinde kwa kishindo.
















 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...