Umoja wa Chama Cha Mapinduzi ( UVCCM) Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma umempongeza Mbunge wa Jimbo hilo Mohammed Monni kwa kutekeleza na kusimamia ipasavyo miradi mbalimbali ya Maendeleo katika Wilaya hiyo Ikiwemo Kufungua shule 13 mpya za Msingi, shule 7 mpya za sekondari, Zahanati 11, pamoja na vituo vya afya.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Umoja huo Mhandisi Jalali Mkunji wakati wakikao cha mwisho wa mwaka cha Bazara hilo kilichofanyika Wilayani hapo.

Mhandisi Mkunji amesema Mbunge Monni amefanyakazi kubwa pamoja na kutoa ushirikiano mkubwa kwa chama chetu pamoja na kuisaidia jumuiya yetu kutimiza wajibu wake.

Amesema jitahidi hizi zimefanikiwa kwa sababu Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ametoa fedha jingi na kuzielekeza maeneo yote ya Nchi yetu.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...