Askari Polisi nchini wametakiwa kuendelea kuchukua hatua kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto ili kudhibiti vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara kwenye jamii.

Rai hiyo imetolewa na Mratibu wa Dawati la Jinsia na Watoto, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Faidha Suleiman akiwa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Wilfred Willa wakati akitoa mada kwa wanafunzi wa kozi ya Uafisa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam Machi 18,2025 huku akiwaonya baadhi ya askari Polisi kutokuwa sehemu ya kutekeleza vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Akitoa mada kwa wanafunzi hao, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Wilfred Willa, amewakumbusha kuhusu wajibu wa afisa wa Polisi katika kushughulikia makosa ya ukati wa kijinsia namna sahihi ya kudhibiti vitendo hivyo kwenye jamii.

Aidha, wanafunzi hao wa kozi ya Uafisa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi wamejengewa uwezo wa kutambua viashiria vya ukatili wa kijinsia, athari za vitendo hivyo, hatua za kuchukua ili kuweza kudhibiti vitendo hivyo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...