Na Mwandishi Wetu

GARNIER ambayo ni mojawapo ya chapa zinazoaminika zaidi duniani katika huduma ya ngozi, imezinduliwa rasmi hapa nchini Tanzania
Uzinduzi wa bidhaa za chapa ya Garnier umefanyika jijini Dar es salaam ambapo imeelezwa hiyo ni  hatua muhimu katika kuleta suluhisho la kisasa, lenye ufanisi, na linalopatikana kwa bei nafuu kwa huduma ya ngozi ya Waafrika.

Akizungumza katika uzinduzi huo Natalie Njenga ambaye ni Kiongozi wa Biashara ya Chapa ya Garnier amesema kuanzia matatizo ya madoa ya rangi usoni, chunusi hadi usawazishaji wa rangi ya ngozi kwa ujumla, Garnier imeleta bidhaa zilizopimwa kitabibu, zenye ushahidi wa kisayansi, zinazotoa matokeo yanayoonekana kwa muda mfupi kwa bei inayomfikia kila Mtanzania. 

"Uzinduzi huu ni hatua muhimu katika kukuza sekta ya urembo nchini Tanzania, ukikidhi mahitaji yanayokua ya huduma ya ngozi bora, nafuu, na jumuishi."

Imeelezwa wakati wa uzinduzi huo kuwa huduma ya ngozi kwa wote katika  msingi wa chapa hiyo  kuna ujumbe wa ujumuishi na kwamba Garnier inatoa suluhisho kwa aina zote za ngozi, rangi na muundo kwa wanawake na wanaume.

Amesema Chapa hiyo  inaamini kuwa huduma ya ngozi si anasa bali ni utaratibu wa kila siku wa kujitunza ambao kila mtu anapaswa kuuweza. Imejengwa Kwa Kusudi Maalum zaidi ya kuwa uzinduzi wa bidhaa, huu ni harakati. 

"Garnier imejidhatiti kwa uwajibikaji wa mazingira—kuanzia vifungashio vilivyotengenezwa kwa kuzingatia mazingira hadi fomula zisizojaribiwa kwa wanyama.

" Zaidi ya hapo, chapa hii imewekeza katika ushirikiano wa muda mrefu na wabunifu wa ndani, vyombo vya habari, wauzaji na jamii kwa ujumla ili kukuza uelewa kuhusu huduma ya ngozi.Huu si uzinduzi tu—ni ahadi,” anasema Njenga.

Kiongozi wa Biashara ya Chapa ya Garnier amesisitiza “Ahadi ya kutoa suluhisho halisi la huduma ya ngozi, lililojengwa kwa sayansi, likitengenezwa kwa uangalifu, na kuzingatia mahitaji ya mlaji wa Kiafrika.”

Bidhaa za Garnier sasa zinapatikana katika maduka ya Shoppers, SH Amon Beauty, Shrijees Supermarket, A-Z Supermarket, Maisha Mart na maduka mengine mengi yatakayoongezwa hivi karibuni.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...