TIMU ya Polisi Tanzania Ijumaa hii Aprili 18, 2025 inawakaribisha Mbeya City katika mchezo wa Ligi ya Championship, mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa Tanzanite Kwaraa Mjini Babati.

Afisa habari wa timu ya Polisi Tanzania Inspekta Frank Lukwaro amesema alama tatu za mchezo huo ni muhimu ikiwemo kulipa kisasi cha kufungwa na Mbeya City katika mchezo wa duru la kwanza katika Uwanja wa Sokoine Mbeya hivyo wameupa umuhimu mkubwa.

Alisema mpaka sasa kikosi hicho kipo vizuri na hakuna majeruhi hivyo kilichobaki ni kuhakikisha kila mchezaji anapambana kuhakikisha wanapata ushindi.

Lukwaro ametoa wito kwa  mashabiki wa timu hiyo mjini Babati  kujitokeza kwa wingi ili kushirikiana kwa kuwa itakuwa siku ya mapumziko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...