KLABU ya Simba imeshindwa kutamba ugenini katika hatua ya robo fainali mkondo wa kwanza dhidi ya Al Masry ya nchini Misri baada ya kupokea kipigo cha mabao 2-0 katika mchezo ambao ulipigwa katika dimba la Suez nchini humo.

Katika mchezo huo licha ya kuutawala mchezo kwa kiwango kikubwa, Simba haikufanikiwa kupata bao katika nafasi nyingi walizozitengeneza kupitia kwa nyota wao, Ateba, Auoa pamoja na Mpanzu.

Al Masry walifanikiwa kupata bao la kuongoza dakika ya 16 ya mchezo kupitia kwa Deghmoum na kufanya kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili Simba waliendelea kulisakama lango la Al Masry bila mafanikio huku Al Masry wakitumia nafasi hiyo kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kufanikiwa kupata bao la pili baada ya kipa wa Simba Sc kufanya harakati za kuokoa krosi na kuwafanya Al Masri kupata baodakika ya 89 ya mchezo.

Simba Sc itasubiri kufanya maajabu katika mchezo wa marudio ambao watakuwa nyumbani Aprili 9,2025 huku ikiwataka kwenye mchezo huo kushinda zaidi ya mabao mawili waweze kufuzu hatua inayofuata.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...