Na John Mapepele 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtaka Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia eneo la Afya  katika Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Prof. Tumaini  Nagu kuhakikisha kwamba huduma ya afya ya msingi inaboreshwa kwa wananchi.

Mhe. Rais ametoa maelekezo hayo leo, Mei 24, 2025  Ikulu ya Dar es Salaam mara baada ya kumuapisha kushika washifa huu baada ya kumteua hivi karibuni.

Mhe. Rais amefafanua kwamba tayari Serikali imeshafanya maboresho makubwa  katika eneo hili kazi iliyobaki ni kuendelea kusimamia kikamilifu ili kuimarisha eneo hili.

" Toka mwaka 2020  Serikali imefanya mambo makubwa  katika eneo hili kuanzia kwenye ukarabati wa zahanati kongwe, vituo vya afya, ongezeko la  vifaa tiba na wataalam". Amesisitiza Mhe. Rais 

Pia Mhe.Rais amemtaka Profesa Nagu kwa kushirikiana na viongozi atakaowakuta  kwenda kutafuta ufumbuzi wa matatizo  ya wananchi kwenye sekta hiyo muhimu kwa taifa letu.

Aidha, amemtaka katika utendaji wa kazi kupunguza urasimu  huku akizingatia miongozo, sheria na kanuni katika utendaji wa kazi.

Katika uapisho huo, Waziri wa  Ofisi ya Rais- TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, Katibu Mkuu, Adolf Ndunguru na Watendaji kadhaa wa Wizara pia wameshiriki.












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...