Na Janeth Raphael MichuziTv -Bungeni Dodoma

KATIKA mwaka wa fedha 2025/2026, Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia idara ya maendeleo ya viwanda imepanga Kukamilisha marejeo na kutekeleza Sera Endelevu ya Maendeleo ya Viwanda pamoja na kuandaa Mpango Kabambe wa Maendeleo ya Viwanda

Hayo yameelezwa leo Mei 14,2025 bungeni na Waziri wa Wizara hiyo,Selemani Jafo wakati akiwasilisha bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Ameyataja mambo mengine ni Kufanya mapitio ya Mkakati wa Ngozi na Mafuta ya Kula; Kuandaa Mpango Kabambe wa Maendeleo ya Viwanda;Kufanya Mapitio ya Sheria ya Chuma Chakavu; na Kuandaa Mkakati na Muongozo wa kuunda na kunganisha magari.

Pia amesema NDC imepanga Kuendelea na utekelezaji wa miradi ya kielelezo ya Mchuchuma, Liganga na mradi wa Magadi Soda Engaruka; Kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya Kimkakati ya Chuma Maganga Matitu, Makaa ya mawe Katewaka; Makaa ya Mawe Mhukuru pamoja na kulipia leseni za uchimbaji.

Vilevile Kuboresha utendaji wa kiwanda cha KMTC ,Kuboresha kiwanda cha Tanzania Biotec Limited kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa ya viuatilifu hai na Mbolea hai na kukamilisha upatikanaji wa Ithibati ya Ubora wa Kimataifa,Kuendelea na ufufuaji wa kiwanda cha Mang’ula.

Pia, Kuendelea na uboreshaji wa miundombinu katika Kongani ya TAMCO na Kange pamoja na kuendeleza eneo la Viwanda la Kimanjaro Machine Tools ili kuvutia wawekezaji Zaidi, Kuendeleza mashamba ya miti ya mpira kwa ajili ya kuzalisha malighafi viwanda na kutunza mazingira,

Vilevile Kuendelea na uboreshaji wa miundombinu ya Shirika ikiwemo ukarabati wa majengo na ofisi, na Kuboresha mfumo wa kitaasisi kwa kuimirisha mifumo ya kisheria, technolojia na kujenga ubobezi wa wataalamu wa shirika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...