Joto la uchukuaji fomu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) linazidi kupamba moto ambapo sasa Ndugu Hamisi Mlaponi amechukua rasmi fomu kwa ajili ya nafasi ya Udiwani katika kata ya Kimang’a, wilayani Pangani, mkoani Tanga.
Mlaponi ni Mwanasayansi katika eneo la Jamii anayejihusisha na masuala ya misaada ya kibinaadamu na kuhamasisha mifumo ya hifadhi ya jamii hususani katika vijiji vilivyopo mkoa wa Tanga.
Pia, kuelekea malengo ya Kidunia ya Maendeleo Endelevu 2030, Mlaponi amadhamiria kutumia ushawishi wa kisiasa katika kuleta mabadiliko chanya kwenye masuala ya Afya, Elimu na Uchumi kwa wakazi wa kata ya Kimang’a
Mbali na hayo Mlaponi pia ameapa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2025-2030 endapo atapata ridhaa ya kuwatumikia wananchi wa Kimang’a na kuwa chachu ya Maendeleo wilayani Pangani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...