Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa TaNESCO ,Irene Gowelle akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana Kampeni ya Tanesco ,jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu,
SHIRIKA la Umeme Tanzania(TANESCO) limesema kuwa watu wenye madeni walipe madeni yao ili Shirika liendelee kujiendesha.
Katika kuwataka wenye madeni kulipa Shirika limeweka kampeni maalum kwenye maeneo yote nchini ya kuhamasisha ulipaji wa madeni kutoka kwa wateja wa malipo ya baada ya ukaguzi wa mita za LUKU kwa wateja wa malipo kabla.
Kampeni hiyo imepewa jina la "Lipa deni,Linda Miundombinu,Tukuhudumie",ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha ulinzi wa miundombinu ya umeme pamoja na juhudi za kuboresha na kuimarisha uendelevu wa upatikanaji huduma bora ya umeme kwa wananchi.
Akizungumza na waandishi habari aarifa Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa TaNESCO ,Irene Gowelle amesema malengo ya kampeni hii ni kuhamasisha wateja wa malipo ya baada ya kulipa madeni yao kwa hiyari kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa na kutoa motisha kwa ulipaji wa wakati ikiwemo msamaha wa riba kwa wateja watakaolipa madeni yao kikamilifu.
"Zoezi hili pia litahusisha ukaguzi wa mita za LUKU kwa lengo la kuhakikisha zinafanya kazi vizuri na hazijachezewa na wateja wasio waaminifu, kauli mbiu yake " Huduma endelevu huanza na wewe",amesema
Aidha ,Kaimu Mkurugenzi Gowelle amesema vile vile kuhamasisha umuhimu wa ulinzi shirikishi wa miundombinu ya umeme kwa kuwajumuisha wananchi na kuwapa elimu ya kulinda miundombinu ya Shirika.Miundombinu hii ndio inayowewezesha upatikanaji endelevu wa huduma ya umeme kwa ufanisi hasa kwa kuzingatia kuwa ulinzi wa Miundombinu ya umma ni wajibu kila mwananchi.
Hata hivyo amesema Shirika linatoa rai kwa wateja wake wote nchini ambao wanadaiwa kutoa ushirikiano kwa kulipa madeni yao kwa wakati na hivyo kutoathiri upatikanaji wa huduma ya umeme kwenye shughulu zao.
Sambamba na hayo Tanesco pia inatoa Rai kwa wananchi kutoa taarifa kuhusu vitendo vya wizi wa umeme au uharibifu na wizi wa miundombinu ya umeme kwa kushirikiana na vyombo vya dola Ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kwa ukosefu wa huduma ya umeme pamoja na kuzuia hasara kwa Shirika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...