
Bendi hiyo yenye sifa za kuwatia wazimu washabiki wa muziki barani ulaya imejizoelea umaarufu kwa kutumia mudundo wake wa muziki wa dansi kutoka Tanzania na Afrika mashariki mrindimo ambao wameupa jina la extraordinary Rhythm "Bongo Dansi" made in Tanzania, mdundo huo wa uliofanikiwa kuwanasa washabiki barani ulaya ,umegeuka kuwa mzimu wa muziki unaotingisha majukwaa kwa takribani miaka 32 tangu kuanzishwa kwa bendi hiyo mwaka 1993 na muhasisi wake mtanzania mwanamuziki Ebrahim Makunja almaarufu Kamanda Ras Makunja.
Tamasha la International Africa Festival Tubingen,Germany ndio onyesho kubwa la kiafrika barani ulaya ambalo linatimiza kuwa onyesho la 25 mwaka huu wa 2025 ambalo linakusanya wajasiliamali,wasanii kutoka nchi mbalimbali za kiafrika ,onyesho hilo ndio gumzo la ulaya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...