Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Prof. Tumaini Nagu amewaelekeza Waganga Wakuu wa Mikoa (RMO`S) Kuhakikisha Hospitali zote za Wilaya Nchini zinalea vituo vilivyopo chini yao ili kufanikisha upatikani wa huduma bora za afya kwenye vituo vyote vya ngazi ya afya Msingi.
Prof. Nagu ametoa maelekezo hayo wakati wa ziara ya usimamizi shirikishi katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.yenye lengo la kuangalia upatikanaji wa huduma za afya, lishe na ustawi wa jamii katika Mkoa huo.
“Waganga Wakuu wa Mikoa wote hakikisheni huduma bora zinazotolewa ikatika hospitali za wilaya, vivyo hivyo hospitali hizo zilee vituo vya afya vilivyopo chini yake navyo viweze kutoa huduma bora na vituo vya afya vitalea Zahanati za maeneo husika” amesisitiza
Aidha, Prof. Nagu amewapongeza Watumishi wa Hospitali ya wilaya ya Mkuranga kwa uhamasishaji mkubwa kwa wananchi wa Mkuranga katika uchangia mkubwa wa damu na kufanya kuwe na hazina ya kutosha.
“Tumeona kuna damu nyingi kwenye majokofu yenu ya kuhifadhia damu na kuna utunzaji mzuri pia katika maabara zenu, na kumekuwa na muitikio mkubwa wa wananchi kuchangia damu hii imetokana na elimu ambayo mmekuwa mkitoa kwa wananchi”
Pia, ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kwa kuwa na maabara bora yenye ithibati ambayo inahakikishia ubora wa majibu ya vipimo hivyo kuwezesha matibabu sahihi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...