Na: Calvin Edward Gwabara – Dar es salaam.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari ameitaka Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini (OCPD) kujitahidi kukamilisha zoezi la ufasili wa sheria zote kwa lugha ya Kiswahili hasa za zile za uchaguzi mkuu na kanuni zake ili zipatikane kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari akipokea zawadi kutoka kwa Bi. Mariam Possi alipotembelea banda la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini (OCPD).

Wito huo ameutoa wakati alipotembelea Banda la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini (OCPD) kwenye maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya SABASABA yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwl Nyerere Jijini Dar es salaama na kutaka kujua mahitaji ya wananchi wayoleta kwenye banda hilo ili waweze kuyafanyia kazi.

“Nafikiri tuendelee kuongeza jitihada katika kazi yetu tunayoifanya ya kufanya ufasili wa  sheria maana kwa kufanya hivyo tutawezesha ufikiwaji wa haki kwa wananchi vizuri hasa hizi sheria za uchaguzi na kanuni zake” Alisisituza Mhe. Johari.

Aidha ameipongeza Ofisi hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa kutoa elimu hiyo kwa umma kupitia maonesho hayo ya sababsaba pamoja na kazi zingine wanazozifanya katika kutekeleza majukumu ya ofisi hiyo waliyopewa kisheria.

Awali Mwandishi wa sheria kutoka OCPD Bi. Mariam Possi alimueleza Mwanasheria Mkuu mambo muhimu ambayo wananchi wanaofika kwenye banda hilo kupata maelezo na kujifunza masula ya mchakato wa utungwaji wa sheria hadi kusainiwa na Rais, namna zoezi la Urekebu wa sheria unavyofanyika na faida zake pamoja na ufasili wa sheria nchini unavyofanyika, ulipofikia na umuhimu wake katika masuala ya utoaji wa haki kwa jamii.

“Katika kipindi chote ambacho tumekuwa kwenye maonesho haya tunapokea wadau wengi wa sheria nchini pamoja na wananchi wenyewe kutoka maeneo mbalimbali ambao wanataka kujua majukumu ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na namna ambavyo wanaweza kuzipata sheria zilizofanyiwa urekebu toleo la mwaka 2023 pamoja na hizi ambazo zipo kwenye hatua ya mwisho za kufanyiwa ufasili kutoka lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili” Alifafanua Bi. Poss.

Mwandishi huyo wa Sheri amesema wanajitahidi kuwaelekeza michakato yote hiyo inavyofanyika kwa umakini lakini kwa kuzingatia sheria na miongozo na kuwaahidi kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria wanaendelea kutumia njia mbalimbali ambazo zitasaidia sheria hizo kuwafikia wananchi popote walipo ili wazisome na kuzielewa na kusaidia jamii kupata haki zao na kujua wajibu wao.

Kauli Mbiu ya maonesho ya 49 ya Kimataifa ya SabaSaba  ni “Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam ‘Sabasaba’ – Fahari ya Tanzania.”

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari akijisajili kidigital kwenye mfumo wa wananchi waliotembelea banda la OCPD kwenye maonesho ya sabasaba.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari akipata maelezo kutoka kwa Bi. Mariam Possi ambaye hayupo pichani wakati akisaini kitabu cha wageni bandani hapo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...