
Hospitali ya Taifa Muhimbili [Upanga & Mloganzila] imeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la watoa huduma za afya katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam [Saba Saba] yaliyohitimishwa leo Julai 13, 2025.
Akizungumza katika sherehe za kufunga Maonesho hayo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amezipongeza taasisi zote zilizoshiriki maonesho hayo na kuzitaka kuongeza juhudi ili kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.
Aidha akikabidhi Tuzo hiyo Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Suleiman Jaffo ameipongeza Hospitali hiyo kwa huduma bora na za kibingwa zinazotolewa kwa wananchi.
Tuzo hiyo imetokana na ubora na utendaji kazi wa wataalam wake waliokuwa wakitoa huduma za kibingwa ambapo wananchi walipata fursa ya kupata elimu, ushauri, uchunguzi na matibabu ndani ya viwanja vya sabasaba.
Kwa upande wa wananchi waliotembelea banda la hospitali hiyo wameishukuru na kuipongeza Muhimbili kwa kuleta hospitali ndani ya maonesho na kusogeza huduma karibu yso kupitia maonesho ya sabasaba.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...