MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, leo Septemba 7, 2025, ameruka kwa helikopta akizisaka kura za kishindo za CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Balozi Dk. Nchimbi ameanza ziara yake ya kampeni Mkoani Kagera kwa kishindo, ambapo atafanya mikutano katika maeneo ya Ngara, Kyerwa, Katoro-Bukoba Vijijini na kuhitimisha kwa mkutano mkubwa Bukoba Mjini.

Katika mikutano hiyo, Dk. Nchimbi atanadi sera na Ilani ya CCM, akieleza mikakati na mipango ya chama hicho endapo kitapewa ridhaa ya kuongoza kwa miaka mitano ijayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...