Farida Mangube, Kilosa
MDAU wa Maendeleo Wilayani Kilosa Ndugu Dotto Ndumbikwa ameahidi kuchangia Madawati Hamsini (50), Magodoro Ishirini (20), Pamoja na Mbao katika Ujenzi wa Shule ya Msingi Mazinyungu Wilayani Kilosa.

Ndugu Dotto ametoa ahadi hiyo wakati akijibu Risala ya Wanafunzi iliyoelezea baadhi ya Changamoto Shuleni hapo katika Mahafali ya kumaliza Elimu ya Msingi kwa mwaka wa 2025.

Kwa upande mwengine Ndugu Dotto amelazimika kufanya harambee kwa wazazi wa Wanafunzi hao ili nao wawe sehemu ya kuchangia katika shughuli za Maendeleo.

Lakini pia Ndugu Dotto amewataka Wazazi na Walezi kusimamia Maadili ya Wanafunzi waliomaliza Darasa la saba ambao muda mwingi kwa kipindi kijacho watakua majumbani, hivyo Wazazi na walezi wanajukumu la kuhakikisha Wanafunzi hao wanabaki katika mstari hadi watakapoingia kidato cha kwanza.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...