Na Said Mwishehe, Michuzi TV
01:KAMPENI zinaendelea kushika kasi na mgombea kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Rais Dk.Samia Suluhu Hassan anaendelea kuchanja mbuga,ameshakwenda mikoa karibia 16 mpaka sasa.
02:Tayari ameshapita katika mikoa ya Dar es Salaam ,Morogoro, Dodoma,Songwe,Mbeya,Njombe,Iringa, Singida,Tabora,Kigoma,Zanzibar,Ruvuma,Lindi,Mtwara,Pwani ,Tanga na leo Kilimanjaro.
03:Kote ambako mgombea Urais amefanya mikutano mikubwa na midogo,amefanya mikutano ya barabarani ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kuzungumza na wananchi na kisha kueleza yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na mipango ya Serikali katika miaka mitano ijayo.
04:Pamoja na hayo kazi kubwa ambayo Dk.Samia Suluhu Hassan anayoifanya katika mikutano ya kampeni ni kuinadi Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030 pamoja na kuomba kura kwa watanzania ili apate ridhaa ya kuwatumikia katika miaka mitano ijayo.
05:Katika kampeni za mgombea Urais Dk.Samia moja ya jambo kubwa ambalo nimeliona ni jinsi ambavyo watanzania wanavyompenda,wanaonesha upendo wa kweli.Watanzania wamekuwa wakijitokeza kwa wingi katika mikutano yake na muda wote wanaona kuna na tabasabu usoni na moyoni.
06:Zipo sababu ambazo zinawafanya Watanzania kujitokeza kwa wingi katika mikutano yake ya kampeni na moja ya sababu ni kwamba Dk.Samia Suluhu Hassan amegusa maisha ya wananchi ,amegusa makundi yote,amegusa sekta sekta zote. Kwa kifupi amegusa maisha ya Watanzajia wote na mimi ni miongoni kwao.
07: Katika miaka miaka minne na nusu ya Dk.Samia Suluhu Hassan kuwa madarakani amegusa maisha ya wakulima wa Taifa hili,kupitia mfumo wa ruzuku katika pembejeo za kilimo wakulima wanaona maisha yao yalivyobadillika.
08:Wakulima wameongeza uzalishaji katika mazao ya chakula na biashara.Kwa Afrika Tanzania inashika nafasi ya pili kwa uzalishaji mahindi na hayo ni matokeo ya mfumo wa ruzuku ambao umeenda kubadilisha maisha ya wakulima wa Taifa hili. Ukienda katika mazao kama mbaazi,korosho,kahawa,chai na mahindi wakulima wanalima kwa kujinafasi.
09:Dk.Samia katika miaka minne na nusu ya uongozi wake amegusa maisha ya watoto wa Taifa hili na hapa nazungumzia mpango wa Serikali wa kutoa elimu bure kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha sita.
10:Serikali ya Rais Samia imebeba jukumu la kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyobora bila kulipa. Kwa elimu ya Vyuo Vikuu, Serikali imeendelea kutoa fedha za mkopo kwa wanafunzi elimu ya juu. Ndio maana wanasema Oktoba 29,2025 wanatiki kwa Samia
11:Ukitaka kujua mgombea Urais kwa tiketi ya CCM amegusa maisha ya watanzania wa makundi mbalimbali zungumza na wafugaji na wakulima ambao walikuwa na migogoro ya ardhi kwa ajili ya kulima na kufuga lakini Dk.Samia amemaliza, migogoro haisikiki tena na kama ipo ni ile inayozungumzika. Sio migogoro ya kushikiana mapanga.Ndio maana wafugaji wanasema watatiki kwa Samia ifikapo Oktoba 29.
12:Katika kipindi cha uongozi wake Dk Samia amefungua milango kwa wananchi kunufaika kupitia rasilimali zilizopo nchini kwa kutekeleza miradi ya kimkakati kama ujenzi wa reli ya kisasa, madaraja, barabara na upanuzi wa bandari za maziwa makuu na baharı.
13:Dk. Samia katika mikutano yake ya kampeni ameendelea kusisitiza umuhimu wa wananchi kutunza amani na utulivu nchini jambo ambalo ndivyo msingi wa maendeleo
14: Siyo hivyo tu kwakuwa ni kiongozi mwenye kuwajali wananchi, ameendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa matumizi ya kupikia ili kulinda afya za wananchi hususan wanawake.
15. Dk. Samia katika uongozi wake ameamua kumtua mama ndoo kichwani na mpango huo utekelezaji wake unafanyika kwa vitendo kupitia miradi mbalimbali ya maji, upatikanaji huduma hiyo kwa nchi nzima umefika zaidi ya asilimia 80
16: Pamoja na yote Dk.Samia Suluhu Hassan ni kiongozi ambaye Mungu amemjalaalia karama ya utu. Ni kiongozi anayeamini katika utu wa mtu ,heshima na kujali na ndio maana katika uongozi wake thamani ya utu wa mtu imepewa nafasi kubwa. Katika uongozi wake hata waliokuwa wamenyimwa haki zao kama kupanda madaraja na kupandishwa mishahara leo wanafufahia.Nao wanasema kwa kulipa Utu huo watatiki Oktoba 29.
17: Kuna mambo yanavutia kwa Dk.Samia pamoja na kuomba ridhaa lakini katika mambo ambayo amekuwa akiyazungumza kwa msisitizo ni mipango yake katika miaka mitano ijayo katika kuhakikisha watanzania wa hali ya kiuchumi nao wanapata hali bora za kiuchumi.Anasema yeye haongozi Wa tanzania wanyonge bali Watanzania wanaoweza kushiriki kikamilifu katika kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
18.Msisitizo wa Dk.Samia kuwa atahakikisha huduma muhimu za kijamii kama maji,umeme,afya,elimu, miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii zinakwenda maeneo ya vijijini yaani kule chini kabisa.Sote tunafahamu maisha ya vijijini kwetu na lengo la Dk.Samia ni kubadilisha kabisa maisha ya vijiji vyetu,ukiona umeme na maji vijijini ujue ndio kazi inaendelea.
19: Ni wakati wa Watanzania sasa kuanza kujiandaa kwenda kupiga kura ifikapo Oktoba 29 mwaka huu na hapa msisitizo wangu sote tuende kutiki kwa Dk.Samia mama mwenye upendo na kubwa zaidi Muumba wa mbinga na ardhi amempa hekima,busara na maarifa.Tusiipoteze nafasi hii,twendeni tukatiki kwa Samia.
20: Jambo kubwa na la mwisho kwa leo ninaloliona kwa Dk. Samia ni ujasiri wake wa kuendeleza diplomasia ya uchumi. Katika kipindi chake amefungua milango ya Tanzania kushirikiana na mataifa mbalimbali duniani, kuimarisha uwekezaji na kuongeza ajira kwa vijana kupitia viwanda na miradi mipya.
Ni Rais anayeamini kuwa Watanzania wana haki ya kunufaika na rasilimali zao kupitia ushirikiano wa kimataifa wa haki. Hivyo Oktoba 29 wananchi wanasema wanatiki kwa Samia ili diplomasia hii iendelee kuwanufaisha.
HITIMISHO
Kwa kuangalia mambo haya 20 niliyoyashuhudia kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka yake minne na nusu ya uongozi na sasa akiwa mgombea urais kupitia CCM, hakuna shaka Watanzania wameona matunda ya kazi yake.
Amegusa kila sekta, ameweka mbele utu wa mwanadamu, ameimarisha diplomasia, ameleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii, huku akisisitiza amani na mshikamano wa Taifa.
Ifikapo Oktoba 29, ni wakati wetu wa kuthibitisha shukrani hizi kwa vitendo kwa kwenda kutitiki kwa Dk. Samia, mama mwenye busara, upendo na dira ya kulipeleka Taifa letu mbele zaidi
KWA WALE WATAKAOTIKI KWA SAMIA OKTOBA 29,2025 BASI TUWASILIANE 0713833822






01:KAMPENI zinaendelea kushika kasi na mgombea kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Rais Dk.Samia Suluhu Hassan anaendelea kuchanja mbuga,ameshakwenda mikoa karibia 16 mpaka sasa.
02:Tayari ameshapita katika mikoa ya Dar es Salaam ,Morogoro, Dodoma,Songwe,Mbeya,Njombe,Iringa, Singida,Tabora,Kigoma,Zanzibar,Ruvuma,Lindi,Mtwara,Pwani ,Tanga na leo Kilimanjaro.
03:Kote ambako mgombea Urais amefanya mikutano mikubwa na midogo,amefanya mikutano ya barabarani ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kuzungumza na wananchi na kisha kueleza yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na mipango ya Serikali katika miaka mitano ijayo.
04:Pamoja na hayo kazi kubwa ambayo Dk.Samia Suluhu Hassan anayoifanya katika mikutano ya kampeni ni kuinadi Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030 pamoja na kuomba kura kwa watanzania ili apate ridhaa ya kuwatumikia katika miaka mitano ijayo.
05:Katika kampeni za mgombea Urais Dk.Samia moja ya jambo kubwa ambalo nimeliona ni jinsi ambavyo watanzania wanavyompenda,wanaonesha upendo wa kweli.Watanzania wamekuwa wakijitokeza kwa wingi katika mikutano yake na muda wote wanaona kuna na tabasabu usoni na moyoni.
06:Zipo sababu ambazo zinawafanya Watanzania kujitokeza kwa wingi katika mikutano yake ya kampeni na moja ya sababu ni kwamba Dk.Samia Suluhu Hassan amegusa maisha ya wananchi ,amegusa makundi yote,amegusa sekta sekta zote. Kwa kifupi amegusa maisha ya Watanzajia wote na mimi ni miongoni kwao.
07: Katika miaka miaka minne na nusu ya Dk.Samia Suluhu Hassan kuwa madarakani amegusa maisha ya wakulima wa Taifa hili,kupitia mfumo wa ruzuku katika pembejeo za kilimo wakulima wanaona maisha yao yalivyobadillika.
08:Wakulima wameongeza uzalishaji katika mazao ya chakula na biashara.Kwa Afrika Tanzania inashika nafasi ya pili kwa uzalishaji mahindi na hayo ni matokeo ya mfumo wa ruzuku ambao umeenda kubadilisha maisha ya wakulima wa Taifa hili. Ukienda katika mazao kama mbaazi,korosho,kahawa,chai na mahindi wakulima wanalima kwa kujinafasi.
09:Dk.Samia katika miaka minne na nusu ya uongozi wake amegusa maisha ya watoto wa Taifa hili na hapa nazungumzia mpango wa Serikali wa kutoa elimu bure kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha sita.
10:Serikali ya Rais Samia imebeba jukumu la kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyobora bila kulipa. Kwa elimu ya Vyuo Vikuu, Serikali imeendelea kutoa fedha za mkopo kwa wanafunzi elimu ya juu. Ndio maana wanasema Oktoba 29,2025 wanatiki kwa Samia
11:Ukitaka kujua mgombea Urais kwa tiketi ya CCM amegusa maisha ya watanzania wa makundi mbalimbali zungumza na wafugaji na wakulima ambao walikuwa na migogoro ya ardhi kwa ajili ya kulima na kufuga lakini Dk.Samia amemaliza, migogoro haisikiki tena na kama ipo ni ile inayozungumzika. Sio migogoro ya kushikiana mapanga.Ndio maana wafugaji wanasema watatiki kwa Samia ifikapo Oktoba 29.
12:Katika kipindi cha uongozi wake Dk Samia amefungua milango kwa wananchi kunufaika kupitia rasilimali zilizopo nchini kwa kutekeleza miradi ya kimkakati kama ujenzi wa reli ya kisasa, madaraja, barabara na upanuzi wa bandari za maziwa makuu na baharı.
13:Dk. Samia katika mikutano yake ya kampeni ameendelea kusisitiza umuhimu wa wananchi kutunza amani na utulivu nchini jambo ambalo ndivyo msingi wa maendeleo
14: Siyo hivyo tu kwakuwa ni kiongozi mwenye kuwajali wananchi, ameendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa matumizi ya kupikia ili kulinda afya za wananchi hususan wanawake.
15. Dk. Samia katika uongozi wake ameamua kumtua mama ndoo kichwani na mpango huo utekelezaji wake unafanyika kwa vitendo kupitia miradi mbalimbali ya maji, upatikanaji huduma hiyo kwa nchi nzima umefika zaidi ya asilimia 80
16: Pamoja na yote Dk.Samia Suluhu Hassan ni kiongozi ambaye Mungu amemjalaalia karama ya utu. Ni kiongozi anayeamini katika utu wa mtu ,heshima na kujali na ndio maana katika uongozi wake thamani ya utu wa mtu imepewa nafasi kubwa. Katika uongozi wake hata waliokuwa wamenyimwa haki zao kama kupanda madaraja na kupandishwa mishahara leo wanafufahia.Nao wanasema kwa kulipa Utu huo watatiki Oktoba 29.
17: Kuna mambo yanavutia kwa Dk.Samia pamoja na kuomba ridhaa lakini katika mambo ambayo amekuwa akiyazungumza kwa msisitizo ni mipango yake katika miaka mitano ijayo katika kuhakikisha watanzania wa hali ya kiuchumi nao wanapata hali bora za kiuchumi.Anasema yeye haongozi Wa tanzania wanyonge bali Watanzania wanaoweza kushiriki kikamilifu katika kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
18.Msisitizo wa Dk.Samia kuwa atahakikisha huduma muhimu za kijamii kama maji,umeme,afya,elimu, miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii zinakwenda maeneo ya vijijini yaani kule chini kabisa.Sote tunafahamu maisha ya vijijini kwetu na lengo la Dk.Samia ni kubadilisha kabisa maisha ya vijiji vyetu,ukiona umeme na maji vijijini ujue ndio kazi inaendelea.
19: Ni wakati wa Watanzania sasa kuanza kujiandaa kwenda kupiga kura ifikapo Oktoba 29 mwaka huu na hapa msisitizo wangu sote tuende kutiki kwa Dk.Samia mama mwenye upendo na kubwa zaidi Muumba wa mbinga na ardhi amempa hekima,busara na maarifa.Tusiipoteze nafasi hii,twendeni tukatiki kwa Samia.
20: Jambo kubwa na la mwisho kwa leo ninaloliona kwa Dk. Samia ni ujasiri wake wa kuendeleza diplomasia ya uchumi. Katika kipindi chake amefungua milango ya Tanzania kushirikiana na mataifa mbalimbali duniani, kuimarisha uwekezaji na kuongeza ajira kwa vijana kupitia viwanda na miradi mipya.
Ni Rais anayeamini kuwa Watanzania wana haki ya kunufaika na rasilimali zao kupitia ushirikiano wa kimataifa wa haki. Hivyo Oktoba 29 wananchi wanasema wanatiki kwa Samia ili diplomasia hii iendelee kuwanufaisha.
HITIMISHO
Kwa kuangalia mambo haya 20 niliyoyashuhudia kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka yake minne na nusu ya uongozi na sasa akiwa mgombea urais kupitia CCM, hakuna shaka Watanzania wameona matunda ya kazi yake.
Amegusa kila sekta, ameweka mbele utu wa mwanadamu, ameimarisha diplomasia, ameleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii, huku akisisitiza amani na mshikamano wa Taifa.
Ifikapo Oktoba 29, ni wakati wetu wa kuthibitisha shukrani hizi kwa vitendo kwa kwenda kutitiki kwa Dk. Samia, mama mwenye busara, upendo na dira ya kulipeleka Taifa letu mbele zaidi
KWA WALE WATAKAOTIKI KWA SAMIA OKTOBA 29,2025 BASI TUWASILIANE 0713833822






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...