Benki ya NMB imefanya kongamano maalum na wafanyabiashara wa mkoa wa Tabora, likilenga kujadili fursa za kifedha na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.

Meneja Mwandamizi wa Idara ya Biashara wa NMB, Dickson Richard, akizungumza katika kongamano hilo lililofanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, amesema benki imejipanga kuendelea kushiri.

kiana kwa karibu na wafanyabiashara katika kuwawezesha kifedha na kukuza biashara zao.

Kongamano hilo limewaleta pamoja wafanyabiashara wa Tabora, likiwa jukwaa la kuimarisha mahusiano na kuonesha nafasi ya benki katika kuchochea ukuaji wa biashara na uchumi wa eneo hilo.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...