Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo Oktoba 7,2025 limepokea ugeni wa Menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) na kufanya kikao Cha kujengeana uwezo ikiwa ni mwendelezo wa juhudi za kuimarisha ushirikiano katika kusimamia na kuhifadhi mazingira nchini

Akifafanua lengo la kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi amesema kimejikita katika kujadiliana mikakati, kutoa ushauri na kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli za mazingira kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hizo na kuongeza tija katika sekta ya mazingira.

Viongozi hao pia wamejadili utekelezaji wa taratibu walizojiwekea katika kufuatilia na kusimamia Sheria za mazingira ili kuhakikisha rasilimali asilia zinatunzwa ipasavyo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa ZEMA, Bw. Sheha Mjaja Juma amesisitiza umuhimu wa wananchi kutimiza wajibu wao kwa kufuata Sheria na taratibu za mazingira, sambamba na Taasisi za maendeleo kuhakikisha miradi yao inazingatia usimamizi endelevu wa mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.

Itakumbukwa kuwa NEMC na ZEMA wamekuwa na mashirikiano ya muda mrefu na mara kadhaa wamekuwa wakitembeleana na kupeana uzoefu kwa maslahi mapana ya Mazingira nchini Tanzania.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...