Na. OWM KVAU – Mbeya

Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed Said, amewataka Vijana nchini kujiwekea utamaduni wa kuweka akiba kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii ili kujihakikishia usalama wa kifedha na ustawi wa maisha yao ya baadaye.

Amesema hatua hiyo itawawezesha vijana kupata huduma muhimu kama mikopo, matibabu, mafao ya uzeeni na fursa nyingine za kiuchumi zinazotolewa na mifuko hiyo.

Mhandisi Zena amebainisha hay oleo Oktoba 13, 2025 wakati akifunga Kongamano la Siku mbili la Vijana, lililofanyika Ukumbi wa City Park Garden Jijini Mbeya.

Aidha, amesema vijana ndio nguvu kazi ya taifa, hivyo ni muhimu kuwekeza katika mustakabali wao kwa kupanga matumizi yao na kujiunga na mifumo rasmi ya hifadhi ya jamii.

“Kijana mwenye utamaduni wa kuweka akiba ni kijana mwenye dira ya mafanikio, anayejali kesho yake na anayechangia katika maendeleo ya taifa,” amesema.

Aidha, amewahimiza vijana kudumisha uzalendo, kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani na kujiepusha na makundi yanayopandikiza chuki au misimamo mikali.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...