WATU 95 wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo uhaini.
Washtakiwa hao wanafanya jumla ya watu waliofikishwa mahakamani hapo kwa siku ya leo ambao wanakabiliwa na kesi za uhaini kuwa 240 ikiwemo Mfanyabiashara Jenifer Jovin ‘Niffer’
Watuhumiwa hao wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkuu, Hassan Makube ambaye ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 19, 2025 kwa ajili ya kutajwa.
Awali wakisomewa mashtaka yao, Imedaiwa kuwa kati ya Aprili Mosi, hadi Oktoba 29,2025 wanadaiwa walikula njama na kupanga kwa siri kufanya kosa la uhaini.
Katila shtaka la pili washtakiwa wote wanadaiwa Oktoba 29, 2025, katika maeneo Sinza ndani ya jiji la Dar es Salaam, wakiwa chini ya utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku wakiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waliunda nia ya kuzuia Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa kutishia mamlaka na kusababisha uharibifu wa mali za serikali.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...