Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameziagiza taasisi za Chuo cha Maji kuongeza juhudi katika kufanya tafiti zitakazosaidia kutatua changamoto za sekta ya maji nchini, zikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa maji na matumizi ya dira za malipo ya kabla (prepaid meters).

Akizungumza leo Novemba 27, 2025 wakati wa mahafali ya 49 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Waziri Aweso alisema jumla ya wahitimu 881 wamemaliza masomo yao mwaka huu, idadi ambayo imeongezeka ikilinganishwa na miaka iliyopita.

Amezielekeza mamlaka za maji nchini kuhakikisha zinatoa nafasi za ajira kwa wahitimu wa fani mbalimbali kutoka Chuo cha Maji, ili kuongeza ufanisi katika uendeshaji na usimamizi wa miradi ya maji mijini na vijijini.

Aweso ameahidi kuendelea kukiimarisha Chuo cha Maji ili kiwe miongoni mwa vyuo vinavyoongoza nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

“Mbali na kuwapatia nafasi wahitimu, pia Wizara itatoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi watano waliofanya vizuri na kupata alama za juu. Tutatoa ufadhili wa Shahada ya Uzamili kwa wanafunzi hao,” alisema Aweso.

Katika mahafali hayo, Waziri Aweso pia alizindua Bodi mpya ya Chuo cha Maji inayoongozwa na Dkt. Maulid Omar, akiitaka kusimamia kikamilifu utendaji wa menejimenti na kutoa ushauri endelevu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Adam Karia, alisema katika mwaka wa fedha 2024/2025 chuo kimefanya mapitio ya mitaala mitatu na kiko katika hatua za mwisho kukamilisha programu mbili za uanagenzi.


















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...