Kaimu Meneja Mgodi wa Barrick Bulyanhulu Leon Ebondo akizungumza wakati Barrick Bulyanhulu Family Day

**
Mgodi wa dhahabu wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga umeandaa tukio la Family Day 2025, ambalo limekutanisha mamia ya wanafamilia wa wafanyakazi wa Mgodi huo ,viongozi wa Serikali na vijiji vinavyozunguka mgodi na wakazi wa eneo hilo ambapo wameungana na kufurahi pamoja.


Tukio hilo ambalo hufanyika kila mwaka mwishoni mwa mwezi Desemba lilipambwa na maonesho ya shughuli zinazofanyika katika mgodi huo, michezo mbalimbali ya watu wazima na watoto, chakula cha pamoja, vinywaji , muziki na kubadilishana mawazo.


Kaimu Meneja Mgodi wa Barrick Bulyanhulu Leon Ebondo ,amewakakaribisha na kuwashukuru wote waliohudhuria hafla hiyo ambayo imewezesha wanafamilia za wafanyakazi kuona kazi zinazofanywa na mgodi sambamba na kudumisha mshikamano na jamii inayozunguka mgodi huo.

Nao baadhi ya wageni waalikwa katika hafla hiyo wamepongeza mgodi huo kwa kuandaa siku hiyo kubwa ambayo mbali na kujumuisha wafanyakazi na familia zao pia inawaunganisha na viongozi wa vijiji jirani na wananchi wanaoishi katika eneo hilo.























Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...