Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Namibia nchini, Mhe. Gabriel Sinimbo, katika tukio lililofanyika katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma, Desemba 10, 2025

Katika mazungumzo yao, Mhe. Dkt. Maghembe amempongeza Mhe. Sinimbo kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo ya kuiwakilisha nchi yake hapa Tanzania na kumhakikishia ushirikiano kutoka Wizarani na Serikalini kwa ujumla wakati wote atakapokuwa akitekeleza majukumu yake ya Ubalozi hapa nchini.

Kwa upande wake, Balozi Mteule, Mhe. Sinimbo amemshukuru Mhe. Maghembe kwa mapokezi mazuri na kueleza dhamira ya Serikali ya Namibia ya kuendelea kukuza ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya mataifa haya mawili.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...