Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 12 Desemba 2025, amepokea tuzo ya kuwa Kivutio Bora cha Mikutano ya Kimkakati Barani Afrika (African’s Best Corporate Retreat Destination 2025). Tuzo hiyo imetolewa baada ya Zanzibar kushinda katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards 2025) zilizofanyika nchini Bahrain.

Mhe. Rais Mwinyi amekabidhiwa tuzo hiyo Ikulu Zanzibar na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), kama ishara ya kutambua mchango na mafanikio makubwa ya Zanzibar katika kukuza sekta ya utalii wa mikutano na matukio ya kimkakati. Ushindi huu umeiweka Zanzibar katika ramani ya dunia baada ya kuibuka kinara dhidi ya mataifa mengine yaliyokuwa yakishindanishwa.

Tuzo hii inaendelea kuthibitisha mageuzi makubwa yanayoendelea katika sekta ya utalii, sambamba na jitihada za Serikali ya Zanzibar kuboresha miundombinu, huduma na mazingira rafiki kwa uwekezaji na mikutano ya kimataifa.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...