Shirika la Masoko ya Kariakoo limeanza rasmi maandalizi ya Mpango Mkakati mpya wa miaka mitano 2026-2031, hatua inayolenga kulifanya soko hilo la kimataifa kutoa huduma bora, kwa wakati na kuzingatia mabadiliko ya teknolojia yanayojitokeza duniani.

Mpango huo unakuja baada ya baada ya mpango wa 2021-2025 kumaliza muda wake wa utekelezaji kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi mafunzo ya uchambuzi na uandaaji wa mpango huo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashiraf Abdulkarim , amesema maandalizi ya mpango huo umeshirikisha wadau ikiwemo Ofisi Waziri Mkuu TAMISEMI, Wafanyabiashara wa Kariakoo, Wapangaji na wadau wengine ili kuwa na mpango mkakati bora, uliochukua mawazo ya wengi na unaojibu matamanio ya kila mmoja na hivyo kuwa rahisi katika utekelezaji wake.

CPA Abdulkarim ameongeza kuwa katika kuandaa mpango huo, Shirika litazingatia nyaraka mbalimbali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050, hotuba ya Rais wakati akifungua Bunge la 13, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa, Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030 pamoja na Sheria na miongozo mbalimbali iliyoanzisha Shirika la Kariakoo.

“Mafunzo haya yatafanyika kwa siku tano na yatakuwa endelevu. Lengo ni kuwa na mpango mkakati bora, unaotekelezeka na unaoweza kupimika kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano ambao utalifanya soko la kariakoo kuwa kinara na linalotoa huduma anuai na sio mazao pekee" amebainisha CPA Abdulkarim.

Amesema mpango huo ukikamilika utalibadilisha soko la Kariakoo kuwa kituo cha kisasa cha biashara, chenye mifumo ya kisasa ya uendeshaji na utoaji huduma.

CPA. Abdulkarim amesema kuwa Kariakoo mpya itakuwa na miundombinu ya kisasa kuanzia maeneo ya maegesho ya magari, mifumo ya kuzima moto, maeneo ya dharura, hewa ya kutosha na mifumo ya kiteknolojia ya uendeshaji. Tunataka kuwahudumia Watanzania katika mazingira bora na ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mipango na Biashara wa Shirika la Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema maandalizi ya mpango huo yanahusisha tathmini ya mpango uliopita wa 2021–2025 ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji maboresho.

Meneja huyo ameongeza kuwa lengo ni kuhakikisha mpango huo unaendana na mikakati ya kitaifa na huku ukilenga kuongeza tija, kuimarisha biashara, na kukuza mchango wa Kariakoo katika uchumi wa taifa.












Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...