Na Mwandishi Wetu

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imeshika nafasi ya pili katika tuzo ya uandaaji na uwasilishaji wa taarifa za mahesabu kwa Viwango vya Kimataifa kwa mwaka 2024 kwa Mamlaka za Udhibiti zilizoshindanishwa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu nchini (NBAA)

Tuzo hiyo imepokelewa na Mkurugenzi wa Fedha  CPA Pascal Karoomba Mkurugenzi wa Fedha kwa niaba yaMkurugenzi Mkuu wa TASAC, Bw. Mohamed Salum 

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya APC Bunju Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Fedha CPA Karomba  wa  amesema ushindi walioupata sio rahisi kwani  taasisi  ni nyingi lakini bado wameendelea kuwa na ubora huku wakijipanga katika kurudi katima nafasi ya kwanza.

Amesema TASAC imeendelea kuchukua ushindi katika nafasi mbambali katika Tuzo za NBAA  katika kipengele cha Mamlaka za udhibiti.

Amesema ushindi huo unaonesha rasilimali walizopewa  na majukumu unaonesha jinsi ambavyo wanawajibika katika utekelezaji wa majukumu yao ambapo wamekuwa wakiyafanya kwa weledi .

Mkurugenzi wa Fedha huyo  meongeza kuwa ili kuwa na maendeleo chanya katika usafirishaji wa majini taasisi yao inatakiwa kufuata misingi Bora ya kimahesabu ambapo hata taasisi za kimataifa zinapotazama
Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) CPA Pascal Karomba akizungumza na Waandishi wa Habari  kwa Niaba ya ya Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salumu  kuhusiana Tuzo ya  Mshindi  Pili ya Uandaaji Tarifa za Fedha mwaka 2024  zinazotolewa na Bodi ya Uhasibu Nchini (NBAA)  katika Hafla iliyofanyika  katika Hotel ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Wakiwa  katika picha mara baada ya kutangazwa washindi wa pili  Tuzo za NBAA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...