Mamlaka ya Mapato tanzania (TRA) yaibuka Mshindi wa Kwanza wa jumla kwenye uandaaji wa hesabu za kifedha zinazozingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu katika Sekta ya Umma (IPSAS). Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) tarehe 4 Desemba, 2025 jijini Dar es Salaam.

Vilevile, TRA imeibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha Taasisi za Serikali (Government Agency Categories) kwenye tuzo hizo.

Aidha, tuzo hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula (Mb.) ambaye alimwakilisha Waziri wa Fedha katika ufungaji wa hafla ya utoaji wa tuzo hizo.

Aidha, katika hafla hiyo jumla ya taasisi 86 za Umma na binafsi mbalimbali zimeshiriki katika kujipima ubora wa kuwasilisha taarifa za fedha kwa mwaka 2024.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...