Waziri wa NchI Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), leo Desemba 10, 2025, jijini Dodoma.
Mazungumzo hayo ni sehemu ya mwendelezo wa mikutano yake na Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo, ikiwa na lengo la kufahamu utekelezaji wa majukumu yao, kusikiliza changamoto, fursa na kutoa maelekezo ya kiutendaji yatakayoongeza ufanisi, uwajibikaji na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika ziara hiyo, Waziri Sangu ameambatana na Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo pamoja na mwakilishi wa Katibu Mkuu Festo Fute, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii.










Mazungumzo hayo ni sehemu ya mwendelezo wa mikutano yake na Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo, ikiwa na lengo la kufahamu utekelezaji wa majukumu yao, kusikiliza changamoto, fursa na kutoa maelekezo ya kiutendaji yatakayoongeza ufanisi, uwajibikaji na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika ziara hiyo, Waziri Sangu ameambatana na Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo pamoja na mwakilishi wa Katibu Mkuu Festo Fute, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii.













Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...