Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amekutana na kuzungumza na Mrajis wa Jumuiya kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Ahmed Khalid Abdulla lengo ikiwa ni kuimarisha utaratibu wa pamoja wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini.

Aidha Mrajis huyo amekutana na kuzungumza na Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s) kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Vickness Mayao wakijikita katika kuweka Mashirikiano kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na utekelezaji wa majukumu yao kwa uwazi, ufanisi na kwa mujibu wa sheria zote mbili.

Kikao hicho cha Robo Mwaka kimefanyika tarehe 29 Januari, 2025 katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma, ambapo pia wamejadili masuala muhimu yanayohusu usajili na usimamizi wa NGOs nchini.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...