Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Kenani Laban Kihongosi, amemuagiza Waziri wa Afya Mhe. Mohamedy Mchengerwa kuhakikisha gari la wagonjwa(Ambulance)linafika katika Hospitali ya Wilaya Singida Vijijini haraka iwezekanavyo.

Alitoa rai hiyo leo Jumatatu January 19 baada ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Singida Vijijini, iliyopo Ilongero, mradi unaogharimu Tsh. bilioni 3.7 katika siku ya pili ya ziara yake ya siku tano mkoani Singida.

Komredi Kihongosi alimpigia simu Waziri wa Afya Mhe. Mohamedy Mchengerwa na kuigiza wizara hiyo kuhakikisha gari hilo linafika kwa wakati.

Gari hili litarahisisha usafiri wa haraka kwa wagonjwa kutoka tarafa tatu zinazotegemea huduma kutoka hospitali hiyo, na hivyo kuondoa usumbufu mkubwa wa huduma ya afya kwa wakazi wa vijiji vilivyombali.














Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...