Na Diana Byera_Bukoba.

Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kagera wameungana na Rais Samia Suluhu Hassan kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda miti 2,000 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Omumwani, Manispaa ya Bukoba.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Mkoa wa Kagera, Faris Buruhani, amewaongoza vijana mbalimbali pamoja na wanafunzi na walimu wa shule hiyo katika zoezi la upandaji miti. Shughuli hiyo pia ilihusisha kukata keki na kuimba nyimbo za kumtakia Rais Samia maisha marefu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti Buruhani alisema vijana wa Mkoa wa Kagera wanamuunga mkono Rais Samia na wanampongeza kwa kazi kubwa anayoifanya, ikiwemo kudumisha amani na mshikamano, kuimarisha uongozi bora, pamoja na kusimamia miradi mbalimbali inayogusa jamii kwa ustadi.

Amesema shule ya wasichana Omumwani imechaguliwa kama sehemu ya kuwatia moyo wanafunzi kutimiza ndoto zao katika masomo na kujiandaa kupata nyadhifa mbalimbali za kuwatumikia wananchi siku za usoni, pia aliwaasa wanafunzi kulinda miti iliyopandwa na kuhifadhi mazingira.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Juliana Rukweto, amevutiwa na uongozi wa mwenyekiti pamoja na mshikamano wa vijana, akisema kuwa hafla hiyo imeacha kumbukumbu ya kudumu, aidha, aliahidi kuendelea kuhamasisha wasichana kusoma kwa bidii na kufanikisha ndoto zao.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...