Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na (Mazingira) wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo Pete (Netiboli) iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
******************
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema itahakikisha uwepo wa Muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar unaendelea kuimarika sambamba na kuibua fursa za ajira kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya michezo.
Hayo yamesemwa leo Alhamisi (Januari 15, 2026) na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Ali Abdulgulam Ali wakati alipokuwa akizindua Ligi ya Taifa ya Muungano katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar.
Mhe. Abdulgulam amesema michezo ni fursa ya ajira kwa vijana wa na hivyo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zitahakikisha zinatumia fursa hizo kuibua vipaji kwa vijana na kuwatengeneza ajira.
“Mashindano haya ni sehemu ya matunda ya Muungano uliojengwa kwa misingi umoja, amani na mshikamano….Serikali zote mbili zitahakikisha zinatumia fursa ya mashindano haya kuwezesha vijana kujitengenezea fursa za ajira” amesema Mhe. AbdulGulam.
Aidha amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itahakikisha inaendelea kushirikiana na Chama cha Netiboli Zanzibar (CHANETA) na Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA)katika kuratibu mashindano hayo ili kuwa nguzo muhimu katika kukuza umoja, upendo na mshikamano kwa Watanzania.
Ameongeza kuwa Serikali zote mbili ztaendelea kuweka mazingira wezeshi kupitia sekta ya michezo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya kisasa katika viwanja mbalimbali hatua inayolenga kuibua vipaji kwa vijana na kutengeneza ajira kwa Kundi hilo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Hanifa Selengiu amesema Serikali zote mbili zimeanzisha mashindano hayo kwa aijli ya kuhakikisha Watanzania wanaendelea kufahamishwa umuhimu wa Muungano na fursa zinazoibuliwa zilizopo ikiwemo sekta ya michezo.
“Mashindano ni utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyotoa mwaka 2024 kuhusu jukumu ilioipatia Ofisi ya Makamu wa Rais ya kuutangaza Muungano” amesema Selengu.
Amesema Michezo ni sehemu muhimu ya Muungano na hivyo mashindano hayo yamekuja katika wakati mwafaka hususani katika kipindi hiki ambacho Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa umma kuhusu Muungano kwa makundi mbalimbali ikiwemo vijana.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Zanzibar (CHANEZA) Bi. Nasra Juma amesema mashindano hayo yameshirikisha jumla ya timu 11 ikiwemo timu sita (06)kutoka Tanzania Bara na tano (05) kutoka Zanzibar.
Amezitaja timu hizo kuwa ni Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Uhamiaji, Tamisemi, Kikosi cha Kujitolea Zanzibar (KVZ), Afya- Zanzibar, Jeshi la Zimamoto, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mbweni, Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA), Polisi Dodoma, Mafunzo na Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU).
Amesema Chama hizo kimeendelea kuweka mikakati mbalimbali katika kuhakikisha Ligi ya ya Netiboli ya Muungano itaendelea kupata washiriki wengi zaidi kwani mchezo huo kwa sasa umezidi kukua na kuweza kufungua milango ya fursa za ajira kwa vijana.
Katika michezo iliyochezwa mapema leo asubuhi Timu ya JKU iliwezesha kupata ushindi wa magoli 36 kwa 34 dhidi ya Polisi Arusha wakati Mafunzo Zanzibar iliiadhibu Timu ya Afya Zanzibar kwa magoli 79 kwa 24.
Watendaji Waandamizi wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)wakifuatilia matukio mbalimbali ya hafla ya uzinduzi Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Pete iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026. Aliyesimama ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Zanzibar, Bi. Shumbana Taufiq.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Hanifa Selengu akiwasilisha salamu za Uongozi wa Ofisi hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli) iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Cecilia Nkwamu akifuatilia matukio mbalimbali ya hafla ya uzinduzi wa Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli)yaliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakipita mbele ya Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Ali Abdulgulam Hussein muda mfupi kabla ya kuzinduliwa kwa wa Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli) iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakipita mbele ya Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Ali Abdulgulam Hussein muda mfupi kabla ya kuzinduliwa kwa wa Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli) iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakiingia katika wa ndani wa Amani Complex, Zanzibar kwa ajili ya kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa Mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli) iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.
Wachezaji wa Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakiwa pamoja na wachezaji wa Timu mbalimbali zinazoshiriki mashindano ya Ligi ya Muungano ya Mchezo wa Pete (Netiboli)iliyozinduliwa leo Alhamisi Januari 15, 2026.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...