Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuweka kipaumbele kikubwa katika uendeshaji wa uchumi, utoaji wa huduma za Taasisi za Umma pamoja na ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mifumo ya kidigitali.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 26 Januari 2026 alipokutana na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Angellah Kairuki, pamoja na watendaji wakuu wa Wizara hiyo, Ikulu Zanzibar.

Amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara za Muungano na Zanzibar, ikiwemo kuharakisha ujenzi wa Kituo cha Ukusanyaji wa Taarifa (Data Centre) Zanzibar, kuboresha miundombinu ya mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa intaneti ya kasi.

Kwa upande wake, Waziri Angellah Kairuki amemhakikishia Rais Dkt. Mwinyi kuwa Wizara yake itaendelea kushirikiana kwa karibu na Zanzibar ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano zilizo salama, za uhakika na zenye viwango vya kitaifa na kimataifa.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...