NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekabidhi jumla ya vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa Taasisi ya Kusimamia Ufundishaji wa Elimu ya Dini ya Kiislamu (TISTA), ikiwa ni hatua ya kuimarisha ufundishaji wa somo hilo katika shule za sekondari nchini.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Januari 11, 2026 katika Ofisi za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) jijini Dar es Salaam, ambapo Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mhe. Abubakar Zuberi, ameupokea mzigo huo wa vitabu kwa niaba ya TISTA akiongozana na viongozi wengine wa taasisi hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesema wamekabidhi nakala 5,000 za vitabu vya kiada vya somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa kidato cha pili vyenye thamani ya shilingi milioni 16, pamoja na nakala 1,000 za vitabu vya mwongozo wa mwalimu vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2, na kufanya jumla ya vitabu vyenye thamani ya shilingi milioni 17.2.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuchapa na kusambaza vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa kidato cha sita pamoja na vile vya kidato cha tatu na cha nne mara tu vitakapokamilika, na kuzipa nakala kadhaa BAKWATA kwa ajili ya kusambaza katika shule zisizo za Serikali Tanzania Bara na Zanzibar.

Aidha, ametoa shukrani kwa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana kwa karibu na TISTA na kufanikisha zoezi la uandishi pamoja na uidhinishaji wa vitabu hivyo.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na madhehebu yote ya dini ili kuhakikisha Elimu ya Dini inafundishwa ipasavyo na kuchangia katika kujenga Mtanzania mwenye maadili mema.

Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mhe. Abubakar Zuberi, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano uliowezesha uandaaji wa maudhui ya vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha malezi na maadili kwa wanafunzi nchini.














Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...