Na. Jacob Kasiri - Zanzibar.
TANAPA kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZCT) watia nanga eneo la Forodhani leo Januari 11, 2026 kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii pamoja na fursa za uwekezaji.
Eneo la Forodhani ni maarufu sana Zanzibar kwa kuwa na wageni kedekede kutoka mataifa mbalimbali kuja kushuhudia shughuli za utalii zinazotekelezwa katika eneo hilo, pia eneo hilo limepokea meli kubwa ya kitalii ya M/S Azamara (Cruise ship) iliyotokea Mauritania ikiwa na watalii 668 na crews 368.
Hivyo uwepo wa TANAPA, TTB sanjari na Kamisheni ya Utalii Zanzibar kama mwenyeji wa eneo hilo ni fursa adhimu na mjarabu ya kunadi vivutio vya utalii kama vile utalii wa wanyamapori na fursa za utalii.
TANAPA wapo Kisiwani Unguja katika Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Dimani - Fumba, Zanzibar, aidha pia shirika hilo linatarajia kushiriki shamra shamra za Sikukuu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar leo usiku kwa kushuhudi urushwaji wa “FASH FASH” itakapotimu saa 6:00 usiku wa leo Januari 11, 2026.
TANAPA kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZCT) watia nanga eneo la Forodhani leo Januari 11, 2026 kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii pamoja na fursa za uwekezaji.
Eneo la Forodhani ni maarufu sana Zanzibar kwa kuwa na wageni kedekede kutoka mataifa mbalimbali kuja kushuhudia shughuli za utalii zinazotekelezwa katika eneo hilo, pia eneo hilo limepokea meli kubwa ya kitalii ya M/S Azamara (Cruise ship) iliyotokea Mauritania ikiwa na watalii 668 na crews 368.
Hivyo uwepo wa TANAPA, TTB sanjari na Kamisheni ya Utalii Zanzibar kama mwenyeji wa eneo hilo ni fursa adhimu na mjarabu ya kunadi vivutio vya utalii kama vile utalii wa wanyamapori na fursa za utalii.
TANAPA wapo Kisiwani Unguja katika Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Dimani - Fumba, Zanzibar, aidha pia shirika hilo linatarajia kushiriki shamra shamra za Sikukuu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar leo usiku kwa kushuhudi urushwaji wa “FASH FASH” itakapotimu saa 6:00 usiku wa leo Januari 11, 2026.









Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...