Na Philipo Hassan - Arusha

Kamishna wa TANAPA, CPA Musa Nassoro Kuji, jana Januari 31, 2026 alipokea tuzo ya “Best Development Partner Supporting Tourism Development” kwa niaba ya Shirika la Korea International Cooperation Agency (KOICA), katika hafla ya utoaji wa tuzo za The Serengeti Awards zilizofanyika katika Hoteli ya Mount Meru jijini Arusha.

Tuzo hiyo alikabidhiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abasi, ikiwa na dhima ya kutambua mchango wa Kituo cha “Serengeti Media Centre” kilichojengwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti kwa ufadhili na ushirikiano wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA).

Lengo la mradi huo ni kuboresha uzoefu wa watalii pindi watembeleapo hifadhi, hususan kituo cha “Serengeti Media Centre”, kwa kuwawezesha kupata picha mjongeo na mnato zinazoonyesha vivutio vya utalii na ikolojia ya Hifadhi ya Taifa Serengeti, hivyo kusaidia katika kuimarisha juhudi za uhifadhi kupitia teknolojia.

Pia, Kamishna Kuji alipata fursa ya kutoa tuzo kwa mshindi wa kipengele cha “Best Conservation Influencer”, ambapo mshindi alikuwa ni Nakaaya Sumari.

Tuzo za Serengeti Awards ni jukwaa adhimu ambalo limeendelea kutambua mchango wa wadau wa utalii na uhifadhi katika maendeleo ya sekta husika, huku zikichochea ubora wa huduma na ubunifu. Kupitia tuzo hizo, Tanzania inaendelea kuimarisha hadhi yake kimataifa kama kinara wa utalii wa safari na wanyamapori katika bara la Afrika na duniani kote.
















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...