Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amekutana na kufanya mazugumzo na Balozi wa India nchini Tanzania Mhe. Bashwadip Dey, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 20 Februari 2026.

Mazungumzo hayo, yamelenga kuimarisha zaidi ushirikiano baina ya India na Tanzania katika sekta mbalimbali za kimkakati. Mahusiano kati ya nchi hizi mbili yamejikita katika sekta ya Afya, Maji, Elimu,Biashara na Uwekezaji pamoja masuala ya Ulinzi na Usalama.

Tanzania na India zina mahusiano mazuri ya kidiplomasia yaliyoanza baada ya Tanzania kupata uhuru ambapo India ilifungua Ubaozi wake mwaka 1961 na Tanzania kufungua Ubalozi wake nchini India mwaka 1962.

Mwaka 2023 mahusiano kati ya nchi hizi mbili yaliongezeka zaidi na kuwa mahusiano ya kimkakati kufuatia ziara rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoifanya nchini India.

India imekuwa na mchango mkubwa katika miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa na Serikali pamoja na kutoa mchango mkubwa katika sekta ya Afya ikiwemo utoaji wa huduma za afya nchini, mafunzo pamoja na Vifaa Tiba.

India imekuwa mdau muhimu wa biashara nchini Tanzania ambapo hadi sasa inashika nafasi ya tatu duniani kwa kufanya biashara na Tanzania. Bidhaa ambazo Tanzania inauza zaidi nchini India ni pamoja na Korosho, karanga, mboga za jamii ya kunde, vito vya thamani na vito vya thamani, pamba; karafuu, chai, Ngozi, mbao na bidhaa za mbao.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...