Kaimu Naibu Kamishna wa Huduma kutoka Idara ya Walipakodi wakubwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Rosemary Ruganuza leo 04.02.2026 Jijini Dar es Salaam katika ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa IDRAS kwa walipakodi wakubwa.

.......

Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani (IDRAS) utasaidia kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza ufanisi wa kazi na kutumia teknolojia ya kisasa katika kusimamia kodi za ndani.

Hayo yameelezwa na Kaimu Naibu Kamishna wa Huduma kutoka Idara ya Walipakodi wakubwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Rosemary Ruganuza leo 04.02.2026 Jijini Dar es Salaam katika ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa IDRAS kwa walipakodi wakubwa.

Bi. Ruganuza amesema lengo la kuwa na mfumo huo ni kuhakikisha muda mwingi wa watumishi unatumika kutekeleza majukumu ya msingi kwa ufanisi.

Ameeleza mfumo wa IDRAS utawezesha utoaji wa huduma zote za usimamizi wa kodi za ndani kwa njia ya kidijitali, jambo litakalorahisisha mawasiliano kati ya TRA na walipakodi pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji.

“Tunataka muda wetu mwingi utumike katika kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi ili mlipakodi asipate usumbufu wowote wakati wa kupata huduma zetu," amesisitiza Bi. Ruganuza

Vile vile amesema mfumo huo wa IDRAS utatusaidia kutoa huduma bora kwa kutumia teknolojia jambo ambalo litarahisisha mlipakodi kutumia mfumo bila kufika ofisi za TRA.

Ameongeza kuwa kupitia IDRAS, walipakodi watanufaika na huduma zilizo rahisi, haraka na salama, huku Mamlaka ikiimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa usahihi na ufanisi zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...