Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza kuanza kwa kampeni maalum ijulikanayo kama “Samia Ardhi Kliniki” itakayofanyika katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026, kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayoadhimishwa tarehe 8 Machi 2026.Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Lucy Kabyemera, amesema kliniki hiyo itaendeshwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi za Ardhi za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.


“Kupitia Samia Ardhi Kliniki tunalenga kuwafikia wanawake wengi zaidi kwa kuwapatia elimu kuhusu haki zao za umiliki wa ardhi, kuwasaidia kitaalamu na kutoa hati miliki kwa waliokamilisha taratibu,” amesema Kabyemera.

Ameongeza kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Samia Suluhu Hassan ya kuwataka watumishi wa umma kuwafuata wananchi na kuwapatia huduma bora kwa kuzingatia utu. “Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,’ na tunawahimiza wanawake wote kujitokeza kutumia fursa hii muhimu,” amesisitiza.
Kwa mujibu wa Kabyemera, serikali inalenga kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi kwani kwa sasa ni takribani asilimia 28 tu ya wanawake nchini ndio wanamiliki. “Tunaamini kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni kuimarisha familia na Taifa kwa ujumla,” amesema.


 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...