Furaha imetanda kwa kinamama wa taasisi ya JAI baada ya kupokea sadaka ya Iftar kutoka kwa taasisi ya Ramadhani Charity Program 2026, ikiwa ni sehemu ya kuendelea kusaidia jamii katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumza wakati wa kukabidhi sadaka hiyo, Mwenyekiti wa Ramadhani Charity Program 2026, Ahmed Misanga, aliwapongeza kinamama wa JAI kwa kuwa mstari wa mbele katika kujitolea na kusaidia jamii.

Misanga alisema kuwa JAI ni washirika wa karibu wa Ramadhani Charity Program, hivyo wameona ni vyema kufika na kuwapatia sadaka ya Iftar kama ishara ya kutambua mchango wao mkubwa katika kusaidia jamii.

Aidha, alitumia fursa hiyo kumuombea dua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na viongozi wengine wa nchi ili waendelee kuiongoza Tanzania kwa amani, umoja na mafanikio.

Kwa upande wake, Kiongozi wa JAI Mkoa, Bi. Aisha Ramadhani, alisema tukio hilo ni faraja kubwa kwao kwani linaonyesha kuwa kazi wanazozifanya za kujitolea zinatambuliwa na kuthaminiwa.

Alimshukuru Ahmed Misanga na Ramadhani Charity Program kwa kuwapatia sadaka hiyo, akisema Allah atawalipa kwa wema huo na wao wataendelea kuwaombea dua kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kusaidia watu wenye uhitaji katika jamii.

Katika hafla hiyo, kinamama wa JAI walipokea msaada wa vyakula vikiwemo tambo, ngano na tende, pamoja na fedha kwa ajili ya mboga kwa ajili ya Iftar.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...