Mtoto mwenye umri wa miaka 12, Rajabu Ally Mohammed, mkazi wa Ijava wilayani Gairo mkoani Morogoro, amefariki dunia kwa kujinyonga baada ya kukemewa na wazazi wake kufuatia tuhuma za kujihusisha na vitendo vya udokozi.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Alex Mkama, amesema tukio hilo limegundulika  Machi 23, 2026 katika kitongoji cha Kaloleni, kata ya Italagwe, ambapo mtoto huyo alikutwa akiwa amejinyonga nyuma ya nyumba yao.

Kwa mujibu wa kamanda wa  Polisi uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Machi 22, 2026 mtoto huyo alikemewa na wazazi wake baada ya kukamatwa pamoja na wenzake wawili wakidaiwa kuiba mahindi mabichi.

 Inadaiwa kuwa kukemewa huko kulimfanya ajisikie vibaya na kuamua kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali yake.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...